Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 19, 2024 Local time: 07:17

Polisi : Mbowe akabiliwa na tuhuma za njama za ugaidi na mauaji


Freeman Mbowe (Facebook/ Freeman Mbowe)
Freeman Mbowe (Facebook/ Freeman Mbowe)

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limesema kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, anakabiliwa na tuhuma mbalimbali ikiwemo za kupanga njama za kufanya vitendo vya kigaidi na kuua viongozi wa Serikali.

Kauli hiyo imekuja baada ya kiongozi huyo wa upinzani kuwa anashikiliwa kwa takribani siku mbili, vyombo vya habari vimeripoti.

Taarifa ya Msemaji wa Jeshi la Polisi, David Misime imesema kuwa kumekuwa na upotoshaji mkubwa kwamba, Mbowe alikamatwa kwa tuhuma za kupanga na kuandaa kongamano la Katiba mpya jijini Mwanza, jambo ambalo si kweli.

“Mbowe alikuwa anafahamu fika kuwa tuhuma zinazomkabili zilikuwa zinachunguzwa na wakati wowote angehitajika Polisi kwa hatua za kisheria mara tu uchunguzi wake utakapokamilika.

Hatua hiyo imefikiwa sasa,” alisema Misime.

Hivi karibuni Mbowe alifanya mkutano na waandishi wa habari na alikosoa kukamatwa kwa wafuasi wa chama hicho na polisi, pamoja na suala la mabadiliko ya katiba.

Chama kikuu cha Upinzani nchini Tanzania, CHADEMA kimesema hakitaendelea kumpigia magoti Rais wa nchi hiyo, Samia Hassan Suluhu kuhusu mustakabali wa taifa hilo, Mbowe aliwaambia waandishi wa habari hivi Jumatatu.

Kauli hii ya Mwenyekiti ilifuatia hatua ya Jeshi la Polisi la nchi hiyo kuwakamata viongozi, wanachama wa chama hicho pamoja na viongozi wa dini 38 waliokuwa wahudhurie mkutano wa chama hicho kupitia baraza lake la vijana (BAVICHA) wenye lengo la kuhamasisha kupatikana kwa katiba mpya ya nchi hiyo.

XS
SM
MD
LG