Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 19, 2024 Local time: 04:58

Pande hasimu Sudan zakubaliana kuwalinda raia na kuruhusu misaada


Wafanyakazi wa kituo cha misaada cha King Salman Humanitarian Aid and Relief load wakipakia mizigo katika ndege ya kijeshi ya Saudi Arabia C130 plane kabla ya kuondoka uwanja wa ndege wa King Khalid kuelekea mji wa Port Sudan, ikiwa Riyadh, Saudi Arabia, Mei 10, 2023.
Wafanyakazi wa kituo cha misaada cha King Salman Humanitarian Aid and Relief load wakipakia mizigo katika ndege ya kijeshi ya Saudi Arabia C130 plane kabla ya kuondoka uwanja wa ndege wa King Khalid kuelekea mji wa Port Sudan, ikiwa Riyadh, Saudi Arabia, Mei 10, 2023.

Pande zinazogombana nchini Sudan zimekubaliana mapema leo kuwalinda raia na upelekaji wa misaada ya kibinadamu lakini hawajakubaliana kuhusu sitisho la mapigano na wako mbali katika hilo , maafisa wa Marekani wamesema.

Baada ya wiki moja ya mazungumzo mjini Jeddah, Saudi Arabia, jeshi la Sudan na kikosi cha RSF wametia saini makubaliano ya kufanya kazi kuelekea katika sitisho fupi la mapigano kwa majadiliano zaidi, wamesema.

Waraka wa makubaliano uliotolewa baada ya mazungumzo umesema pande hizo mbili zimeweka nia ya dhati ya kuweka kipaumbele kwa majadiliano ya kufanikisha sitisho la muda mfupi la mapigano ili kufanikisha upelekaji wa misaada ya dharura ya kibinadamu na kurudisha huduma muhimu.

Taarifa ya wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema pande hizo mbili zitazingatia zaidi kufikia makubaliano ya sitisho la mapigano litakalofanya kazi kwa kiasi cha siku kumi.

Wapatanishi wanafanya kazi na Saudi arabia na marekani wanaosimamia majadiliano hayo baadaye watazungumzia hatua maalumu za usalama kwa ajili ya ulinzi wa vifaa vya misaada, afisa wa Marekani amesema.

Hata hivyo Washington inategemea pande hizo mbili kukubali kutia saini makubaliano hayo kutajenga nguvu zaidi .

XS
SM
MD
LG