Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Februari 13, 2025 Local time: 09:10

Misri yakataa pendekezo la Israel la uangalizi wa eneo lisilo na silaha


Moshi ukifuka huko Khan Yunis wakati Israel ilipofanya mashambulizi kutoka Rafah Desemba 25,2025. Picha na SAID KHATIB / AFP)
Moshi ukifuka huko Khan Yunis wakati Israel ilipofanya mashambulizi kutoka Rafah Desemba 25,2025. Picha na SAID KHATIB / AFP)

Misri imekataa pendekezo la Israel la kutaka kuwa mwangalizi mkuu wa eneo lisilo na silaha kati ya mpaka wa Misri na Gaza, na kuzipa kipaumbele juhudi za usimamizi wa sitisho la mapigano kabla ya kushughulikia mipango ya baada ya vita, vyanzo vitatu vya usalama vya Misri vimesema.

Misri inashirikiana mpaka wa kilometa 13 na Gaza, ni mpaka pekee uliopo katika pwani ya Palestina ambao haudhibitiwi moja kwa moja na Israel.

Pamoja na Qatar, Misri pia ina jukumu la kuongoza mazungumzo katika kusimamia sitisho jipya la mapigano huko Gaza na kufanikisha makubaliano ya kuachiliwa mateka wa Israel wanaoshikiliwa na Hamas.

Vyanzo vya Misri vimesema wakati wa mazungumzo hayo Israel iliieleza Misri kuhusu uimarishaji wa njia ya Philadelphi, eneo jembamba lisilo na silaha kwenye mpaka, kama sehemu ya mipango ya Israel kuzuia mashambulizi ya baadaye.

Mgogoro wa sasa umeanza Oktoba 7, wakati Hamas ilipoanya uvamizi ambapo Israel imesema watu 1,200 waliuawa na wengine wapatao 240 kuchukuliwa mateka.

Israel imelipiza kisasi Israel imelipiza kisasi kwa mashambulizi

yaliyoua zaidi ya watu 23,000, kulingana na maafisa wa Gaza, na kuwafanya watu zaidi ya milioni 2.3 kuzikimbia nyumba zao.

Forum

XS
SM
MD
LG