Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Januari 19, 2025 Local time: 07:42

Viongozi mashariki ya kati wamedhamiria kuzuia mgogoro wa Gaza; Asema Blinken


Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Antony Blinken
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Antony Blinken

Mustakabali wa eneo hilo unahitaji kuwa moja ya muingiliano, sio mgawanyiko na sio migogoro, alisema Blinken.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Antony Blinken amesema Jumatatu viongozi wa Mashariki ya Kati wamedhamiria kuzuia mgogoro wa Gaza kuenea na kwamba kuna utambuzi mpana juu ya haja ya "kuweka njia ya kisiasa kwa Wapalestina.

Ukingo wa Magharibi na Gaza zinapaswa kuungana kuwa chini ya utawala wa Palestina, Blinken aliwaambia waandishi wa habari katika uwanja wa ndege wa Al Ula nchini Saudi Arabia.

Mustakabali wa eneo hilo unahitaji kuwa moja ya muingiliano, sio mgawanyiko na sio migogoro, alisema Blinken, akiongeza ili hilo litokee, tunahitaji kuona kuanzishwa kwa taifa huru la wa-Palestina.

Forum

XS
SM
MD
LG