Al -Faqi al -Mahdi alihukumiwa na mahakama hiyo mwaka jana kwa kuharibu masanamu 9 na mlango wa msikiti wakiwa na silaha na matrekta makubwa.
Uhalifu huo ulitokea katika mji wa zamani wa kihistoria wa Timbuku, wakati wenye msimamo mkali walipochukua udhibiti kwa muda mfupi kaskazini mwa Mali mwaka 2012.
Katika maamuzi ya kihistoria mahakama iliamua uharibifu huo wa masanamu kuwa ni uhalifu wa kivita wakati ilipomhukumu Al -Mahdi miaka 9 jela.
Alikuwa anaweza kupata miaka 30 jela lakini mahakama ilifikiria kuhusu suala lake la kukubali makosa na kuonyesha kusikitishwa.