Kwa siku ya tatu chama cha Republikan kimeshindwa kumchagua Spika wa kuongoza Baraza la Wawakilishi Marekani. Kiongozi wa chama hicho ameshindwa kupata kura za kutosha. Shinikizo linaendelea. Ijumaa mzunguko wa 12 wa kumchagua spika wa baraza la wawakilishi Marekani umeanza na hakuna mgombea yeyote aliyepata kura 218 zinazohitajika. Wabunge 435 wa Marekani wameanza mzunguko wa 12 kumchagua spika wa baraza la wawakilishi ambapo hakuna matumaini kwa Kevin McCarthy kupata ushindi licha ya kufanikiwa kuongeza kura chache kutoka kwa wapinzani wake. Endelea kusikiliza historia ya uchaguzi wa Spika wa Marekani na yale ambayo yanatarajiwa kutokea kutoka kwa mchambuzi wetu. Endelea kusikiliza...
Matukio
-
Machi 05, 2024
Je, nini Super Tuesday?
-
Machi 05, 2024
Misaada ya kimataifa yaanza kuwasili Sudan
-
Februari 12, 2024
Polisi wapambana na waandamanai Kinshasa
-
Februari 06, 2024
Polisi wavambia bunge la Senegal na kuwaondoa wabunge wa upinzani.