Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 12:49

Makerere yapoteza kiongozi muhimu katika safu yake


Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Ukaguzi ya Chuo Kikuu cha Makerere, Uganda na naibu mwenyekiti wa Mamlaka ya Mipango ya Taifa, marehemu Dr Abel Rwendeire atapewa heshima zote za kiserikali wakati wa maziko yake Jumapili.

Wakati wa ibada maalum iliyofanyika katika eneo la Kumbukumbu ya Mashujaa huko Namugongo Ijumaa, Waziri Mkuu Dr Rwendeire aligusia kuwa Dr Rwendeire atazikwa kiserikali Jumapili katika mji wa wazee wake huko Kibuzigye, Wilaya ya Rubanda.

“Hivi sasa bunge liko mapumzikoni, lakini mara litapoanza shughuli zake kutakuwa na mswada wa kuruhusu waheshimiwa Wabunge kutoa heshima zao kwa Dr Rwendeire,” alieleza.

Waziri Mkuu ambaye alikuwa amefuatana na Naibu Waziri Mkuu wa pili Kirunda Kivejinja na maafisa wa ngazi ya juu wa serikali, alitoa maombolezo juu ya waziri mkuu huyo aliyeaga dunia na kusema kuwa “ni mwanasayansi adimu sana, mwanasiasa, kiongozi na mwanazuoni.

Marcy Rwendeire, mjane wa marehemu, alimuelezea mumewe kama ni mtu mwenye upendo na kuahidi kuchukua jukumu la kuwasimamia na kuwatunza watoto wao sita.

“Mume wangu aliaga dunia ghafla. Tulikuwa tumekaa tunaangalia televisheni pale aliponiambia kuwa anahisi maumivu kwenye kifua yanaongezeka,” alieleza, na kuongeza kuwa ilikuwa wakati wa asubuhi wakati alipogundua kuwa mumewe hawezi kuongea.

Majirani zetu walitusaidia kumpeleka hospitali lakini tulipofika tukaambiwa tayari ameaga dunia,” amesema.

Mkewe amesema kuwa alikutana naye mwaka 1978 Chuo Kikuu cha Makerere na walikuwa washerehekee miaka 40 ya ndoa yao mwaka 2018.

Mary Kobusingye Oyuru ambaye alizungumza kwa niaba ya watoto wa marehemu alisema baba yao alikuwa “ni mfano wa kuigwa na wengine.”

“Alitufundisha mambo mengi na kutupa elimu bora kabisa na hivyo kutuwezesha sote kupata shahada za juu,” alieleza.

XS
SM
MD
LG