Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 27, 2024 Local time: 03:27

Mahakama Uingereza yazuia muasisi wa Wikileaks kupelekwa Marekani


Watu wakisheherekea uamuzi wa Jaji wa kutompeleka muasisi wa WikiLeaks Julian Assange Marekani, wakiwa nje ya Mahakama, London, Uingereza , Januari 4, 2021. REUTERS/Henry Nicholls
Watu wakisheherekea uamuzi wa Jaji wa kutompeleka muasisi wa WikiLeaks Julian Assange Marekani, wakiwa nje ya Mahakama, London, Uingereza , Januari 4, 2021. REUTERS/Henry Nicholls

Mashabiki wa Julian Assange, mchapishaji na muasisi wa mtandao wa Wikileaks waliokua nje ya mahakama mjini London wamefurahia uamuzi wa Jaji Vanessa Baraitser wa Uingereza wa kutompeleka Marekani kukabiliwa na mashtaka ya ujasusi, kwa kuchapisha waraka za siri kwenye mtandao wake.

Jaji Baraister anasema amechukua uamuzi huo kutokana na hatari ya uwezekano wa Assange kujiua.

Jaji huyo ameeleza kwamba endapo Assange atapelekwa Marekani ambaye ni Muaustralia atakabilwa na hali ya kushikiliwa katika mazingira magumu ya kumtenganisha na watu na mawasiliano na watu wa nje na hivyo kumuathiri kiakili na kwa hiyo aliamrisha asipelekwe Marekani.

Assange mwenye umri wa miaka 49 anaendelea kushikiliwa hadi pale ombi lake la kuachiliwa kwa dhamana litaposikilizwa Jumatano.

Waendesha mashtaka wa Marekani na Uingereza wanaweza kukata rufaa kutokana na uamuzi huo. Mawakili wake wametoa hoja kwamba kesi dhidi yake ina malengo ya kisiasa.

XS
SM
MD
LG