Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Aprili 28, 2025 Local time: 18:08

Rais Magufuli awataka watendaji polisi, Takukuru kuwatendea haki wananchi


Rais wa Tanzania, John Magufuli
Rais wa Tanzania, John Magufuli

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli Alhamisi ameamrisha ofisi ya mkurugenzi wa mashtaka (DPP), mwanasheria mkuu (AG) na ofisi ya jaji kiongozi kutafuta ufumbuzi wa kesi za mjane aliyejitokeza katika sherehe za siku ya Sheria.

Rais Magufuli wakati akizindua mwaka mpya wa kimahakama nchini unaojulikana kama siku ya sheria alishtukia hekaheka za walinda usalama wakimzuia mama huyo aliyejitambulisha kwa jina la Swabaha Mohamed ambaye ni mkazi wa mkoa wa Tanga.

Mwandishi wa Idhaa ya Kiswahili ameripoti kuwa Magufuli aliwashukia watendaji wa polisi na taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (Takukuru) kwa madai ya kukwamisha uendeshaji na hukumu za kesi mbalimbali na pia kuvuruga ushahidi.

“Mnakwenda mahakamani mnazungumza upelelezi bado unaendelea, umemshika na jino la tembo, unasema upelelezi unaendelea unataka umshike na nini tena kingine,” rais alihoji.

“Umemshika na madawa ya kulevya, upelelezi unaendelea, mara nyingine yale madawa yanabadilishwa yakishafikishwa kwa mkemia mkuu yalikuwa madawa ya kulevya yakageuzwa kuwa mihogo kutoka sumbawanga…,” alisema.

please wait

No media source currently available

0:00 0:03:00 0:00
Kiungo cha moja kwa moja

Mjane huyo amedai kudhulumiwa haki yake ya mirathi ya marehemu mume wake alizua taharuki ghafla katikati ya uzinduzi huo na kutoa malalamiko yake moja kwa moja kwa rais, huku akiwa na vielelezo vya kesi anazodai zimechukua muda mrefu, huku kukiwa na njama pia za kumtoa uhai ili kumdhulumu haki yake.
Uzinduzi wa mwaka mpya wa mahamaka umebeba kauli mbiu ya 'umuhimu wa utoaji haki kwa wakati utakavyowezesha ukuaji wa kiuchumi'.

Taasisi hizo tatu zimetakiwa kushughulikia mara moja kesi ya mjane huyo aliyejitokeza katika mahafali ya siku ya sheria nchini.

“Kama kesi iko mahakama ya mwanzo muivute kutoka huko haraka haraka na ishughulikiwe mara moja,” Rais alitoa amri hiyo.

Pia aliitaka ofisi ya mkuu wa polisi (IGP) ishughulikie kesi hiyo na kumlinda mjane huyo asije akadhulumiwa kwa kitu chochote.

XS
SM
MD
LG