Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 14:42

Lupita naye amlalamikia Weinstein


Harvey Weinstein
Harvey Weinstein

Mcheza filamu na mshindi wa tuzo ya Oscar Lupita Nyong’o, raia wa Kenya, amejitokeza kuungana na wacheza sinema wengine kadhaa wanawake waliotoa shutuma za udhalilishaji wa kingono dhidi ya mzalishaji maarufu wa filamu wa Hollywood Harvey Weinstein.

Katika Makala iliyochapishwa kwenye majarida kadha ikiwa ni pamoja na gazeti mashuhuri la New York Times.Nyong’o anaeleza uamuzi wake wa kusimulia kisa kilichomkuta hivi sasa akiungana na sauti za wanawake wengine ambao walikuwa wamebughudhiwa na kudhalilishwa kimapenzi.

“Nilikuwa nimeweka dukuduku langu dhidi ya Harvey mbali kabisa na akili yangu, na kujiunga na wale waliokubaliana kunyamaza dhidi ya uovu huu ambao umempa nafasi mwindaji huyu wa ngono kuwadhalilisha wanawake kwa miaka mingi. Nilikuwa najihisi niko peke yangu wakati udhalilishaji huu ulipotokea, na nilijilaumu kwa yaliyotokea, kama vile ilivyokuwa kwa wanawake wengine ambao wamesimulia dukuduku lao.

Lakini kwa vile hivi sasa suala hili linazungumziwa kwa uwazi sikuweza kujizuilia na kumbukumbu zangu juu ya udhalilishaji huu zilizojitokeza. Nilijisikia ndani ya tumbo langu kuwa ninaumwa. Nilihisi vile hasira zinavyonipanda ni kitambua kuwa simulizi yangu siyo ya kipekee bali ni sehemu ya mfumo wa kitabia.”

Weinstein inadaiwa kuwa kwanza alijaribu kumlazimisha Nyong’o wawe na mahusiano wakati alipojitokeza kutathminiwa katika shindano la filamu katika makazi yake mzalishaji huyo huko Westport, Connecticut. Wakati huo Nyongo alikuwa bado ni mwanafunzi wa Sanaa ya kuigiza chuo cha Yale. Nyong’o anaelezea:

“Harvey alinipeleka chumbani- chumbani kwake- na akatangaza kuwa alikuwa anataka kunifanyia massage (kunikanda). Nilidhani kuwa alikuwa anatania hapo awali. Ilikuwa siyo hivyo. Kwa mara ya kwanza tangu nikutane naye nilijihisi siko salama. Nilishtuka kidogo na kufikiria haraka jinsi ya kumuepuka na kuweza kujihami nafsi yangu, kujua hasa sehemu gani mikono yake ilikuwa inataka kushika wakati wote huo.

Muda siyo mrefu alisema anataka kuvua suruali yake. Nilimwambia asifanye hivyo na kuwa itanifanya niwe katika hali ya taharuki… nilifungua mlango na kusimama kwenye kizingiti. Alivaa shati lake na mara nyengine alisema jinsi nilivyokuwa mjeuri. Nilikubaliana naye huku nikicheka na kujaribu kuondokana na hali hiyo kwa salama.”

Kama Nyong’o anavyoeleza, sehemu ya mafunzo yake ilikuwa ni kujifunza namna ya kukanda na mazoezi ya viungo, lakini Weinstein amedai vitendo hivyo vilionyesha kuvuka mstari. Baadae, anaeleza jinsi alivyopitia katika mchakato wa kutambua jinsi atavyoweza kulishughulikia suala hili kwa umakini zaidi—“Nilikuwa naingia katika biashara ambayo mahusiano mazuri ni sehemu ya weledi na kwa hivyo kunajichanganya sana,” amesema. Baadae ameandika juu ya tukio – akiwa katika chakula cha usiku na kundi la watu—pamoja na Weinstein ambapo alimgundua kuwa ni mtu mwenye “mashara na ucheshi.” Bila shaka alikuwa ni mdhalilishaji, lakini pia anaweza kuwa mcheshi kweli kweli, kitu ambacho kilikuwa kinachanganya na kuvutia.” Nyong’o amesema.

Lakini baada ya kukutana naye mara kadha katika shughuli za kikazi za kawaida, Nyong’o anasimulia kukutana kwao katika chakula cha usiku ambapo alijikuta yuko peke yake na Weinstein (Nyong’o anasema kuwa msaidizi wake husubiri mpaka anapofika na kuondoka). Weinstein alimtongoza kwa mafumbo:

Kabla ya chakula cha utangulizi kufika [Weinstein] alisema: Twende katika mchezo. Nina chumba changu binafsi juu ambapo tunaweza kupata sehemu ya chakula cha usiku iliyobakia.

Nilishtuka. Nilimwambia nilikuwa napendelea kula katika mgahawa. Akaniambia acha utoto wako.

Iwapo nataka kuwa muigizaji, ni lazima niwe tayari kufanya vitu kama hivi. Alisema alikuwa ametembea na Muigizaji Maarufu X na Y na angalia wamefikia wapi katika fani hii.

Nyong’o ameandika kuwa “kwa upole alikataa pendekezo hilo” na kumshangaza Weinstein—anadai kuwa Weinstein alimwambia kuwa “ hatambui fursa gani anaipoteza

Baada akiendelea kupiga hatua katika fani hii ya uigizaji, na baada ya Nyong’o kuwa nyota katika filamu inayoitwa 12 Years a Slave, ambayo alipata tuzo ya Academy, Weinstein alimfuata Nyong’o baada ya tafrija ya sherehe hiyo huko Toronto. Weinstein alimwambia Nyong’o alikuwa anaona fedheha katika nafsi yake kwa kile alichomtendea na kuahidi kuwa atamheshimu kuanzia hapo. “Lakini niliweka ahadi moyoni kwamba sitafanya kazi na Harvey Weinstein milele,” ameongeza Nyong’o.

Na hiyo ndiyo ilikuwa mara ya mwisho kukutana pamoja, Nyong’o amesema haraka sana kwamba yuko mbali na mtu pekee katika sekta ya filamu ambaye ametumia madaraka yake kinyume cha sheria.

XS
SM
MD
LG