Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, hafla hiyo imefanyika kimya kimya kinyume na siku za nyuma labda kutokana na malalamiko mengi yaliowasilishwa na upinzani, pamoja na baadhi ya mataifa ya kigeni, kuwa uchaguzi uliofanyika Agosti 9 ulikuwa na udanganyifu.
Upinzani hata hivyo umepuuzia kuapishwa kwa Lukashenko na badala yake kutaka maandamano dhidi ya utawala wake yaendelee na ambayo yamekuwa yakifanyika kwa wiki 6 sasa.
Marekani pamoja na Umoja wa Ulaya wanaendelea kutathmini kuhusu vikwazo dhidi ya maafisa waliohusika kwenye uchaguzi huo pamoja na maafisa wa usalama ambao wamekuwa wakifanya misako dhidi ya waandamaji.
Baada ya kuapishwa, Lukashenko mwenye umri wa miaka 66 amesema kuwa taifa lake linahitaji usalama na maelewano wakati likikabiliana na janga la kimataifa, akionekana kuashiria janga la virusi vya corona.