Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 16:07

Lipumba: tume ya uchaguzi ndio tatizo kubwa


Profesa Ibrahim Lipumba kiongozi wa chama cha upinzani CUF Tanzania
Profesa Ibrahim Lipumba kiongozi wa chama cha upinzani CUF Tanzania

Prof Lipumba kiongozi wa CUF anasema wananchi wamechoshwa na maisha magumu lakini tume ya uchaguzi ni tatizo kwa upinzani kuweza kupata ushindi.

Vyama vikuu vya upinzani huko Tanzania vinadai kwamba wananchi wamechoshwa na maisha magumu pamoja na sera za chama tawala cha CCM.

Mgombea kiti cha rais kwa niaba ya chama cha CUF Profesa Ibrahim Lupumba akizungumza na Sauti ya Amerika amesema kutokana na mahitaji makubwa ya wananchi kwa wakati huu ni muhimu sana kukuza uchumi na kuongeza ajira.

Ili kufikia malengo hayo anasema "inahitaji kuwekeza katika miundo mbinu hususan kua na umeme wa hakika,na umeme uweze kusambazwa katika vijiji vikubwa vikubwa kusudi watu waweze kupata fursa kuanzisha viwanda vidogodogo vinavyoweza kutoa ajira", amesema kiongozi wa chama cha wananchi CUF, Profesa Lipumba.

XS
SM
MD
LG