Wachambuzi wanasema hatua hiyo ilikuwa imechelewa.
Vita vya ndani kati ya 1989 na 2003 ilishuhudia ukatili mkubwa ikiwa ni pamoja na mauaji, ubakaji, na matumizi ya askari watoto.
Baadaye Kamati ya Ukweli na Maridhiano iliitaka mahakama maalum iundwe kuwasikiliza wanaodaiwa kuhusika.
Hata hivyo, hakuna hatua madhubuti zilizochukuliwa hadi Boakai alipochaguliwa mwaka jana. Rais huyo alipendekeza azimio la kuunda mahakama maalum, ambalo baadaye liliungwa mkono na bunge la chini la Liberia na seneti.
Siku ya Alhamisi, Boakai aliwashukuru wabunge kwa kazi yao na akatoa idhini yake ya mwisho.
Forum