Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 09, 2025 Local time: 07:43

Kiwanda cha nishati cha Ukraine chashika moto kufuatia shambulizi la drone la Russia


Moto kwenye kiwanda cha Trypilsaka karibu na Kyiv Alhamisi. Reuters Aprili 11, 2024
Moto kwenye kiwanda cha Trypilsaka karibu na Kyiv Alhamisi. Reuters Aprili 11, 2024

Russia katika siku za karibuni imefanya  mashambulizi makubwa ya anga na ndege zisizokuwa na rubani kwa  raia  wa Ukraine  na miundo mbinu ya nishati na kusababisha  vifo na uharibifu mkubwa.

Mashambulizi mapya ya Ijumaa yalilenga kituo cha nishati katika mkoa wa kusini wa Dnipropetrovsk, ambacho kimepata uharibifu mkubwa baada ya kushika moto kutokana na shambulizi la droni la mapema leo, jeshi la Ukraine na afisa wa mkoa wamesema.

Mkuu wa mkoa huo Serhiy Lysak amesema kuwa wafanyakazi wa zima moto wa Ukraine walifanikiwa kuuzima moto huo, ingawa kiwango cha uharibifu hakikuweza kukadiriwa mara moja. Wakati huo mkuu wa mkoa wa Kherson, Oleksandr Prokudin amesema kuwa mashambulizi ya usiku kucha ya Russia katika mkoa wa kusini mwa Ukraine yameharibu miunjdo mbinu ya kiwanda muhimu ambacho hakijatajwa.

Prokudin amesema kwamba maeneo 15 ya makazi kwenye mkoa huo pia yalishambuliwa, lakini hakuna vifo vilivyo ripotiwa ingawa nyumba kadhaa ziliharibiwa. Ripoti zimesema kwamba mifumo ya ulinzi wa anga ya Ukraine imetungua droni 16 kati ya 17 zilizorushwa na Russia katika mikoa sita, jeshi la Ukraine limesema mapema kupitia ujumbe kwenye mitandao ya kijamii.

Forum

XS
SM
MD
LG