Kabila amesema kwamba ripoti hiyo ilimharibia jina.
Ripoti hiyo ya shirika la habari za uchunguzi la Ufaransa – Mediapart, kwa ushirikiano na shirika lisilo la kiserikali la kuwalinda watu wanaotoa habari za siri Afrika, inataja Kabila na watu kutoka ukoo katika kashfa ya wizi wa mamilioni kadhaa ya dola.
Wakili wa Kabila Raphael Nyabirungu amesema kwamba watafungua kesi mahakamani.
Washirika wa karibu wa Joseph Kabila wamedai kwamba rais huyo wa Zamani ni mtu mwadhilifu anayependa sana taifa lake na aliyefanya kazi kwa heshima na taadhima na kwa hivyo watamtetea kwa njia zote.