Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Februari 16, 2025 Local time: 22:30

Ghasia Sudan Kusini zauwa raia 166


Hali ya utapiamlo nchini Sudan Kusini iliyosababishwa na vita na ukame. Regina Williams akipimwa katika kituo cha Afya cha Nyong kuthibitisha iwapo ana utapiamlo.
Hali ya utapiamlo nchini Sudan Kusini iliyosababishwa na vita na ukame. Regina Williams akipimwa katika kituo cha Afya cha Nyong kuthibitisha iwapo ana utapiamlo.

Ghasia huko Sudan Kusini katika jimbo la Upper Nile zimeuwa raia 166 na kuwakosesha makazi zaidi ya watu 20,000 tangu mwezi Agosti wakati mapambano yaliposambaa kati ya makundi yenye silaha,  Kamishna wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Binadamu alisema Jumatano.

Ghasia zimeongezeka katika sehemu za Sudan Kusini ambako mapambano yamechochewa na mizozo ya ndani juu ya maeneo ya malisho ya mifugo, maji, ardhi za kilimo na rasilmali nyingine ambapo mara kwa mara hali huchochea mapambano mabaya.

Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi wiki iliyopita lilisema mzozo unaoendelea ambao ulianza mwezi Agosti katika kiijiji kimoja huko Upper Nile, tangu wakati huo umesambaa katika sehemu nyingine kwenye jimbo hilo na maeneo kadhaa kwenye majimbo ya Jonglei na Unity.

XS
SM
MD
LG