Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Julai 27, 2024 Local time: 04:10

Umoja wa Mataifa: Watu milioni 7.8 Sudan Kusini wanaweza kukabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula


Mwanamke ameshika mbegu za Lilies kwenye ambazo anatumia kutengeneza supu, huko Old Fangak katika jimbo la Jonglei, Sudan Kusini Desemba 28, 2021.
Mwanamke ameshika mbegu za Lilies kwenye ambazo anatumia kutengeneza supu, huko Old Fangak katika jimbo la Jonglei, Sudan Kusini Desemba 28, 2021.

Hadi kufikia watu milioni 7.8 nchini Sudan Kusini, theluthi mbili ya watu wote, wanaweza kukabiliwa na uhaba mkubwa wa chakula katika msimu wa mwaka ujao wa Aprili hadi Julai kutokana na mafuriko, ukame na migogoro, mashirika ya Umoja wa Mataifa yalisema Alhamisi.

Uhaba huo ni mbaya zaidi kuliko kilele cha vita vya wenyewe kwa wenyewe vya mwaka 2013 na 2016, Shirika la Chakula na Kilimo, Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto UNICEF na Mpango wa Chakula wa Umoja wa Mataifa (WFP) walisema.

“Kupungua kwa usalama wa chakula na kuenea kwa utapiamlo kunahusishwa na mchanganyiko wa migogoro, hali mbaya ya uchumi, hali mbaya ya hewa, na kuongezeka sana kwa gharama za chakula na mafuta," walisema katika taarifa.

"Wakati huo huo, kumekuwa na kupungua kwa ufadhili wa programu za kibinadamu licha ya kuongezeka kwa mahitaji hayo ya kibinadamu." Waliongeza.

Ongezeko la bei za vyakula duniani lililochochewa na uvamizi wa Russia nchini Ukraine, muuzaji mkubwa wa nafaka nje, kuliacha mashirika ya kibinadamu na upungufu wa fedha za wahisani.

XS
SM
MD
LG