Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 17:03

Ghasia Darfur zawalazimisha watu 15,000 kukimbia makazi yao


FILE - Wanawake wakibeba maji katika kambi ya wakimbizi waliokimbia vita katika mji mkuu wa Al Geneina, magharibi ya Darfur, June 29, 2011.
FILE - Wanawake wakibeba maji katika kambi ya wakimbizi waliokimbia vita katika mji mkuu wa Al Geneina, magharibi ya Darfur, June 29, 2011.

Ghasia zilizoanza tena katika mkoa wa Darfur nchini Sudan zimesababisha vifo na kukoseshwa makazi kwa zaidi ya watu 15,000 wiki iliyopita UN imesema.

Taarifa ya UN imesema mzozo binafsi baina ya wanaume wawili kutoka kabila la Masalit na wahamaji wa Kiarabu wamesababisha ghasia karibu na mji wa El Geneina.

Kundi la Nomad lililokuwa na silaha lilivamia soko la ndani na kuchoma moto sehemu ya kijiji na kuua watu tisa wakiwemo watoto wawili.

Mapigano pia yamesababisha watu 4,000 kukimbilia katika mpaka wa Chad.

Zaidi ya watu milioni mbili bado wanaishi katika kambi kutokana na matokeo ya mzozo wa Darfur katika miaka ya 2000.

Mwaka 2021 umeshuhudia ghasia mpya huko Darfur kukiwa na mashambulizi ya mara kwa mara katika vijiji yanayofanywa na wanamgambo.

XS
SM
MD
LG