Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 20, 2024 Local time: 11:22

Abiria 239 wawasili Kenya wakitokea China


Abiria wakiwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa King Khalid, Riyadh Saudi Arabia, Januari 29, 2020, kutoka China na maafisa wa afya wakiwapima kuhakikisha hawana kirusi cha corona. REUTERS/Ahmed Yosri - RC2VPE9TZQ8X
Abiria wakiwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa King Khalid, Riyadh Saudi Arabia, Januari 29, 2020, kutoka China na maafisa wa afya wakiwapima kuhakikisha hawana kirusi cha corona. REUTERS/Ahmed Yosri - RC2VPE9TZQ8X

Maafisa wa serikali ya Kenya Jumatano wamewaruhusu abiria 239 ambao waliwasili katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta mjini Nairobi wakiwa ndani ya ndege ya China Southern.

Abiria wote walifanyiwa uchunguzi maalum wa kiafya na baadaye kuruhusiwa kuingia nchini humo.

Wakati huohuo Wizara ya Afya imesema abiria walishauriwa kujitenga kwa muda wa siku 14 kama hatua ya tahadhari dhidi ya uwezekano wa kusambaza virusi vya corona.

Hii ni mara ya kwanza kwa idadi kubwa ya abiria kuambiwa kujitenga na watu wengine.

Waziri wa Afya, Sicily Kariuki amesema katika taarifa yake kwamba kesi 17 za washukiwa wa virusi vya corona zimeripotiwa nchini humo, lakini wote waliofanyiwa uchunguzi wa kiafya wamegundulika hawajaambukizwa virusi hivyo.

Hata hivyo amewaasa raia wa Kenya kutofanya safari ambazo si muhimu kwenda kwenye nchi ambazo zimethibitishwa kuwa zina kesi za virusi vya corona.

Wakenya wengi wamestushwa na uamuzi wa serikali kuruhusu abiria kutoka China kuingia nchini.

Imetayarishwa na mwandishi wetu, Washington, DC.

XS
SM
MD
LG