Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Machi 28, 2024 Local time: 22:01

Wakazi wa Mwanza wajitokeza kuuaga mwili wa hayati Magufuli

Maelfu ya wakazi wa Mwanza na maeneo jirani wamejitokeza kuupokea mwili wa hayati John Pombe Magufuli katika Uwanja wa Ndege wa Mwanza na kuusindikiza mwili huo mpaka Uwanja wa CCM Kirumba ambapo shughuli ya kuuaga inafanyika.

Wananchi wa Kirumba, Ghana, Kiloleli, Nyasaka, Buzuluga, Mabatini, Mwanza mjini, Igogo, Mkuyuni, Nyegezi, Mkolani, Buhongwa na Usagara wakiwa wamesimama barabarani kumuaga aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika awamu ya tano Hayati Magufuli wakati akipitishwa katika mitaa mbalimbali ya Jiji la Mwanza mara baada ya kuagwa katika uwanja wa CCM Kirumba, Jumatano, Machi 24, 2021.
Picha kwa hisani ya Global Publishers TV na Ofisi ya Rais, Tanzania.

Pandisha zaidi

Makundi

XS
SM
MD
LG