Abiy Ahmed aliteua mawaziri 20 katika baraza jipya la mawaziri na kumi ya hao ni wanawake
Mabadiliko ya baraza jipya la mawaziri nchini Ethiopia yaliyofanywa wiki hii na waziri mkuu Abiy Ahmed yamepongezwa na wanaharakati wa haki za wanawake nchini humo. Waziri mkuu Abiy katika mabadiliko hayo aliteua mawaziri 20 na kumi ya hao ni wanawake na baadhi yao wamepewa wizara muhimu.