Wachunguzi wa Uturuki waliendelea na msako wao kwenye ubalozi wa Saudi Arabia
Wachunguzi wa Uturuki hivi leo waliendelea na msako wao kwenye ubalozi mdogo wa Saudi Arabia mjini Istanbul na kwenye nyumba ya karibu ya ubalozi huo ili kufahamu nini kilimtokea mwandishi wa habari, Jamal Khashoggi. Khashoggi hajulikani alipo tangu alipoingia ubalozini hapo Oktoba mbili.