Idadi ya vifo imeongezeka kutokana na maporomoko ya matope ambayo yalilikumba eneo la Mount Elgon nchini Uganda linalopakana na Kenya. Mamia ya wenyeji katika eneo hilo wamekoseshwa makazi kutokana na nyumba zao kuharibiwa na mvua kubwa, iliyokuwa inanyesha kwa siku kadhaa mfululizo.