Jeshi la Kenya lilifanya operesheni Alhamisi kuwaokoa wahanga wa mvua kubwa iliyosababisha vifo vya darzeni za watu kote Afrika Mashariki katika muda wa mwezi mmoja uliopita.
Wakulima wa Sudan Kusini ambao wamekuwa wakiyategemea mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayofanyakazi nchini humo sasa wanasema wanahofia kupoteza soko lililopo tayari kwa mazao yao, iwapo Umoja wa Mataifa utatekeleza tishio lake la kupunguza operesheni zake katika taifa hilo changa duniani.
Serikali ya Marekani na baraza la Kitaifa la Kulinda Nchi huko Niger (CNSP), Balozi wa Marekani nchini Niger Kathleen Fitz Gibbon na Meja Jenerali Ken Ekman, Mkurugenzi wa Mikakati, Ushirikiano na Mipango wa Kamandi ya Marekani ya Afrika, watakutana na maafisa wa baraza hilo.
Jeshi la Afrika Kusini litaongeza muda wa kutumwa kwa wanajeshi wake katika nchi zilizokumbwa na mzozo Msumbiji na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Rais Cyril Ramaphosa alisema katika taarifa yake siku ya Jumatano.
Muigizaji na balozi wa ukarimu wa Umoja wa Mataifa Danai Gurira amewaambia wanadiplomasia siku ya Jumanne kuwa kumpata mtoto kutoka katika unyanyasaji wa kingono katika maeneo ya kivita kunagharimu chini ya dola moja.
Mamlaka ya Ufaransa inasema msichana mwenye umri wa miaka 7 alikuwa miongoni mwa wahamiaji watano waliozama kwenye mfereji wa bahari kati ya Uingereza na Ufaransa, maarufu English Channel,
Benki ya Dunia ilisema Jumanne kuwa imesitisha ufadhili wa mradi wa utalii na uhifadhi nchini Tanzania kufuatia madai ya ukiukwaji wa haki za binadamu.
Watu kadhaa waliangamia katika maafa mapya ya boti ya wahamiaji kwenye pwani ya Djibouti, shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa lilisema Jumanne.
Mamlaka nchini Zimbabwe imechukua hatua ya haraka kuhusiana na kushuka hivi karibuni kwa sarafu ya dhahabu inayoungwa mkono, kwa kuwakamata wanaofanya magendo ya kubadilisha fedha na kufunga akaunti za biashara zinazotuhumiwa kutumia dola za Marekani peke yake.
Maafisa wawili wa ngazi ya juu wa Uingereza Jumanne wameomba serikali ifikirie tena mpango wake wa kuwapeleka waomba hifadhi nchini Rwanda, wakionya kuwa hatua hiyo huenda ikawa ni matokeo mabaya kwa haki za kibinadamu pamoja na usalama wa wakimbizi.
Chama tawala nchini Afrika Kusini cha African National Congress -ANC kilishindwa katika kesi ya pili mahakamani dhidi ya chama kipya cha upinzani kinachoongozwa na aliyekuwa Rais Jacob Zuma siku ya Jumatatu.
Aharon Haliva ni afisa wa kwanza wa ngazi ya juu Israel kujiuzulu kuhusiana na shambulio la oktoba 7 la hamas dhidi ya Israel.
Pandisha zaidi