Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Mei 03, 2024 Local time: 21:57

Maafisa wa ngazi ya juu wa UN washauri Uingereza dhidi ya kupeleka wahamiaji Rwanda


Kamishna wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia haki za binaadamu Volker Turk, akiwa Geneva Decemba 11, 2023. Picha na REUTERS/Denis Balibouse
Kamishna wa Umoja wa Mataifa anayeshughulikia haki za binaadamu Volker Turk, akiwa Geneva Decemba 11, 2023. Picha na REUTERS/Denis Balibouse

Maafisa wawili wa ngazi ya juu wa Uingereza Jumanne wameomba serikali ifikirie  tena mpango wake wa kuwapeleka waomba hifadhi nchini Rwanda, wakionya kuwa hatua hiyo huenda ikawa ni matokeo mabaya kwa haki za kibinadamu pamoja na usalama wa wakimbizi.

Katika taarifa ya pamoja, Fillippo Grandi kamishna wa shirika la wakimbizi la Umoja wa Mataifa, na Volker Turk kamishna wa haki za binadamu kwenye Umoja huo, wameishauri Uingereza badala yake ishughulikie wimbi la wahamiaji na wakimbizi wanaoingia nchini humo.

Grandi amesema kuwa sheria mpya ya Uingereza inakwenda kinyume na utamaduni wake wa kutoa hifadhi kwa wanaohitaji, ikikiuka mkataba wa kimataifa wa wakimbizi. Turk awali alilalamikia mpango huo amesema kuwa unahujumu utawala wa sheria wa Uingereza na mfano mbaya kwa ulimwengu.

Jumatatu waziri mkuu wa Uingereza Rishi Sunak aliahidi kuanza kupeleka waomba hifadhi nchini Rwanda ndani ya kati ya wiki 10 hadi 12 zijazo.

Forum

XS
SM
MD
LG