Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Mei 05, 2024 Local time: 21:37

Uganda: Mahakama yapinga rufaa ya wapenzi wa jinsia moja kutaka usajili


Wapenzi wawii wa jinsia moja nchini Uganda wakijifunika na bendera ya kujivunia ushoga, Machi 25, 2023. Picha ya AP
Wapenzi wawii wa jinsia moja nchini Uganda wakijifunika na bendera ya kujivunia ushoga, Machi 25, 2023. Picha ya AP

Mahakama ya Uganda Jumanne ilitupilia mbali rufaa ya kundi la kutetea haki za wapenzi wa jinsia moja lililotaka usajili wa serikali, na kuamua kwamba kundi hilo lina lengo la kuendeleza shughuli “haramu”.

Mahakama ya rufaa ilisema usajili wowote wa kundi la Sexual Minorities Uganda (SMUG) ni kinyume na maslahi ya umma na sera ya kitaifa.

Walalamishi walitaka jina hilo lisajiliwe “ kwa madhumuni ya kuimarisha haki za ngono za watu walio wachache wanaojulikana kama LGBTQ,” aliamua Jaji Catherine Bamugemereire kwa niaba ya jopo la majaji watatu.

Wanaharakati walikuwa wanakata kusajili SMUG kama kampuni ndogo ili kuiwezesha kufanya kazi kihahali nchini Uganda, ambapo vitendo vya mapenzi ya jinsia moja vimeharamishwa.

Forum

XS
SM
MD
LG