Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Mei 21, 2024 Local time: 05:43

Shambulio la kombora laua wanajeshi watatu wa Tanzania wa kikosi cha SADC nchini DRC


Wakazi wanaokimbia mapigano katika wilaya ya Masisi, wakusanyika karibu na magari ya wanajeshi wa Afrika Kusini wanaojumuika katika kikosi cha SADC mashariki mwa DRC, Februari 7, 2024. Picha ya AFP
Wakazi wanaokimbia mapigano katika wilaya ya Masisi, wakusanyika karibu na magari ya wanajeshi wa Afrika Kusini wanaojumuika katika kikosi cha SADC mashariki mwa DRC, Februari 7, 2024. Picha ya AFP

Shambulio la kombora mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo liliua wanajeshi watatu wa Tanzania ambao walikuwa katika kikosi cha SADC kilochopelekwa huko kusaidia wanajeshi wa serikali ya DRC kupambana na waasi wa M23, maafisa walisema.

Kikosi hicho cha SADC kilipeleka wanajeshi katika jimbo la Kivu Kaskazini mwezi Disemba kusaidia serikali ya Kinshasa kudhibiti tena maeneo yaliyotekwa na waasi wa M23 mashariki mwa nchi.

Kikosi hicho kinajumuisha wanajeshi wa Afrika Kusini, Tanzania na Malawi.

“Tukio hili la kusikitisha lilitokea baada ya kombora la adui kuanguka karibu na kambi ya wanajeshi hao,” taarifa ya kikosi cha SADC ilisema.

Haikutoa maelezo zaidi kuhusu tukio hilo.

Forum

XS
SM
MD
LG