Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Mei 18, 2024 Local time: 10:48

Shambulio la bomu laua watu tisa katika kambi ya wakimbizi mashariki mwa DRC


Waasi wa kundi la M23 wakilinda eneo hilo wakati wa mkutano kati ya maafisa wa Kikosi cha Afrika Mashariki (EACRF) na waasi wa M23 katika kambi ya Rumangabo huko DRC Januari 6, 2023. Picha na Guerchom Ndebo/AFP
Waasi wa kundi la M23 wakilinda eneo hilo wakati wa mkutano kati ya maafisa wa Kikosi cha Afrika Mashariki (EACRF) na waasi wa M23 katika kambi ya Rumangabo huko DRC Januari 6, 2023. Picha na Guerchom Ndebo/AFP

Milipuko iliwaua watu tisa Ijumaa katika kambi ya wasiokuwa na makazi yao nje kidogo ya mji wa Goma katika eneo linalokumbwa na vita mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, vyanzo katika eneo hilo vimesema.

“Mabomu” yalianguka kwenye vibanda ambavyo ni nyumba za wasiokuwa na makazi, kulingana na mashahidi, katika eneo la mashariki mwa nchi, ambalo limeshuhudia mapigano yanayoendelea kati ya waasi wa M23 na serikali.

Chanzo cha milipuko ya Ijumaa hakijafahamika wazi. Kwa mujibu wa mashahidi, wanajeshi wa serikali walio karibu na kambi hiyo wamekuwa wakiwashambulia waasi kwenye milima ya eneo la mbali magharibi mwa nchi tangu asubuhi, kulingana na mwanaharakati wa mashirika ya kiraia, “M23 walilipiza kisasi kwa kurusha makombora kiholela”.

Msemaji wa serikali Patrick Muyaya amelishutumu kwenye mtandao wa X “jeshi la Rwanda na waasi wa M23” kwa kuhusika na shambulio hilo.

Kulingana na serikali ya Congo, Umoja wa mataifa na nchi za Magharibi, nchi jirani ya Rwanda inawaunga mkono waasi wa M23, madai yanayokanushwa na Kigali.

Waasi wa M23 wamekanusha pia kwamba hawakuhusika na shambulio hilo na kulishtumu jeshi la DRC kwa kurusha mabomu hayo.

Forum

XS
SM
MD
LG