Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Mei 04, 2024 Local time: 12:25

Mashirika ya haki za binadamu yasema watu 118 waliuawa na polisi wa Kenya mwaka 2023


Picha hii inaonyesha mwanamke akibeba vitu vyake kichwani, akipita kando ya matairi yalichomwa katika mtaa wa Kibera, Nairobi, Machi 30, 2023 wakati wa maandamano ya upinzani. Picha ya AFP
Picha hii inaonyesha mwanamke akibeba vitu vyake kichwani, akipita kando ya matairi yalichomwa katika mtaa wa Kibera, Nairobi, Machi 30, 2023 wakati wa maandamano ya upinzani. Picha ya AFP

Jumla ya watu 118 walikuwa waathirika wa mauaji holela yaliyotekelezwa na polisi wa Kenya mwaka uliopita, makundi ya haki za binadamu ya ndani na ya kimataifa yamesema katika ripoti iliyochapishwa Jumatano, yakilaani “kutowajibishwa” kwa maafisa wa usalama waliohusika katika mauaji hayo.

Idadi hiyo imeshuka kwa asilimia 9 ikilinganishwa na watu 130 waliouawa mwaka 2022, huku idadi ya watu waliotoweka ikipungua kwa zaidi ya asilimia 50 katika kipindi hicho, ripoti hiyo imesema.

Nusu ya mauaji hayo yalifanyika wakati wa operesheni za kupambana na uhalifu, kulingana na ripoti ya mashirika ambayo ni pamoja na Human Rights Watch, Amnesty International Kenya na kundi la Kenya la Missing Voices.

Watu wengine 45 waliuawa wakati wa maandamano yaliyoitishwa na upinzani nchini Kenya kati ya mwezi Machi na Julai mwaka jana kupinga gharama ya juu ya maisha, mashirika hayo yamesema.

Msemaji wa polisi Resila Onyango hakujibu ombi la shirika la habari la AFP la kutoa maelezo kuhusu ripoti hiyo.

Forum

XS
SM
MD
LG