Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Aprili 20, 2025 Local time: 17:03

Zelensky atembelea Romania


Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy, amekwenda Bucharest, Jumanne kukutana na mwenzake wa Romania, Klaus Iohannis, ambapo walijadili uhusiano wa nchi hizo mbili huku Russia, ikiendelea na uvamizi wake Ukraine.

Mkutano huo ni wa kwanza wa Zelensky, nchini Romania, tangu uvamizi wa Russia, Februari mwaka jana.

Romania, mwanachama wa Umoja wa Ulaya na NATO, imekuwa ikiunga mkono juhudi za vita vya Ukraine, huku rais Iohannis akisema kuwa nchi yake inalenga kuisaidia Ukraine, kushinda vita.

Zelenskyy, alisisitiza uhusiano thabiti wa mataifa hayo mawili na kuishukuru Romania, kwa kuendelea kuiunga mkono kijeshi na kibinadamu.

Zelenskyy amesema kwenye mtandao wa X, kwamba uhusiano wa nchi hizo mbili ni muhimu kwa utulivu kwa Ulaya na kwingineko.

Forum

XS
SM
MD
LG