Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Aprili 26, 2024 Local time: 23:06

Zambia inakaribisha mazungumzo na makampuni yake ya madini


Vifaa vya uchimbaji shaba
Vifaa vya uchimbaji shaba

Wizara ya fedha ya Zambia ilisema Jumapili kwamba ipo wazi kuzungumza na makampuni ya madini nchini humo juu ya mipango ya serikali ya kuongeza kodi ya madini.

Zambia ni nchi ya pili kwa ukubwa barani Afrika kuzalisha shaba ilisema mwishoni mwa mwezi uliopita kwamba itatangaza majukumu mapya yanayohusu shughuli za madini na kuongeza kodi ili kusaidia kupunguza kiwango cha deni kwa nchi hiyo.

Kulingana na shirika la habari la Reuters wachimbaji wakubwa wa madini kama vile kampuni ya First Quantum, Glencore na Vedanta Resources mara kwa mara wanaikosoa serikali ya Zambia kwa kuongeza gharama kwenye operesheni zao za uchimbaji madini nchini humo.

XS
SM
MD
LG