Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 15, 2025 Local time: 14:27

Zaidi ya wakimbizi 100,000 wawasili Armenia wakikimbia mapigano katika eneo la Azerbaijan la Nagorno Karabakh


Wakimbizi wa kabila la Armenia kutoka eneo la Nagorno Karabakh waonekana katika mji wa Goris Septemba 30, 2023.
Wakimbizi wa kabila la Armenia kutoka eneo la Nagorno Karabakh waonekana katika mji wa Goris Septemba 30, 2023.

Zaidi ya wakimbizi 100,000 waliwasili nchini Armenia kutoka eneo la Nagorno-Karabakh, mkuu wa shirika la Umoja wa mataifa linalohudumia wakimbizi (UNHCR) alisema Ijumaa.

“Wengi wana njaa, wamechoka na wanahitaji msaada wa haraka,” alisema Filippo Grandi kwenye mtandao wa kijamii.

Grandi aliongeza kuwa “ UNHCR na washirika wengine wa kutoa misaada ya kibinadamu wameongeza msaada wao kwa mamlaka za Armenia, lakini msaada wa kimataifa unahitajika kwa haraka.”

Jeshi la Azerbaijan wiki iliyopita lilivamia na kuchukua udhibiti wa eneo linalokaliwa na watu wa kabila la Armenia na kusababisha wimbi la ghafla la wakimbizi.

Armenia Jumamosi imesema zaidi ya watu 100,000 kati ya idadi ya watu wanaokadiriwa kuwa sawa na 120,000 walikimbia tangu eneo hilo lililojitenga kushuhudia mapigano dhidi ya utawala wa Azerbaijan kwa miongo kadhaa, na mapigano hayo kumalizika ghafla kwa kushindwa.

Forum

XS
SM
MD
LG