Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 22:46

Zaidi watu 35 wauawa na wanamgambo kaskazini mashariki mwa DRC


Makamanda wa kundi la wanamgambo la CODECO wakitembea kwenye kijiji cha Linga mkoani Ituri, January 13, 2022. Picha ya AFP
Makamanda wa kundi la wanamgambo la CODECO wakitembea kwenye kijiji cha Linga mkoani Ituri, January 13, 2022. Picha ya AFP

Washambuliaji wameua watu 35 akiwemo mtoto mchanga katika shambulio kwenye mgodi wa dhahabu katika mkoa wa Ituri kaskazini mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo, vyanzo vya eneo hilo vimesema Jumapili.

Jean Pierre Bikilisende, afisa kwenye eneo la vijijini la Mungwalu wilayani Djugu, katika mkoa wa Ituri, amesema wanamgambo wa kundi la CODECO walifanya shambulio hilo kwenye mgodi huo.

Bikilisende amesema wanamgambo hao waliushambulia mgodi wa dhahabu wa Camp Blanquette na kwamba maiti 29 ziliondolewa huko, huku maiti nyingine sita zilizochomwa moto zimekutwa zimezikwa kwenye eneo hilo.

Miongoni mwa waliouawa kuna mtoto mwenye umri wa miezi minne, ameongeza.

Cherubin Kukundila, kiongozi wa kiraia huko Mungwalu, amesema takriban watu 50 waliuawa katika shambulio hilo.

XS
SM
MD
LG