Ikiwa njia moja ya kukamilisha mwezi wa wanawake,viongozi wanawake kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wametoa wito kwa wenzao kujiunga na vyama vya kisiasa na kushiriki kwenye uchaguzi ikiwa njia moja ya kujipatia uongozi na kushiriki kwenye maswala ya Serikali.
Wanawake hao wameombwa kushiriki kwenye uongozi kwa madai kuwa walieko madarakani wameshindwa na majukumu yao hasa kuleta Amani kaskazini mwa DRC ambapo michafuko ya mara kwa mara imekuwa ikitokea kama anavyosimulia Austere Malivika kutoka DRC.