Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 28, 2025 Local time: 09:25

WHO yasema kuwa njia zaidi za uokozi kutoka Gaza zinahitajika


Mwanamke wa Kipalestina akishika mkono wa mtoto wakati wagonjwa wa saratani wakisubiri kuokolewa kutoka Ukanda wa Gaza, Aug. 15, 2024.
Mwanamke wa Kipalestina akishika mkono wa mtoto wakati wagonjwa wa saratani wakisubiri kuokolewa kutoka Ukanda wa Gaza, Aug. 15, 2024.

Afisa wa ngazi ya juu wa Shirika la Afya Duniani WHO, huko Gaza amesema Alhamisi  kuwa njia zaidi  za kutoka zinahitajika ili kufanya uokozi wa kimatibabu kwa maelfu ya Wapalestina wakiwemo watoto ambao wanahitaji missada ya kuokoa maisha.

“Kunahitaji kuwa na jinsi ya kuwawezesha wagonjwa zaidi kupitia Rafah kuingia Misri, lakini pia tunahitaji njia nyingine,” Dkt Rik Peeperkorn aliambia wanahabari kwa njia ya video kutoka Gaza. “Njia ya kwanza ambayo tungependa kuona ikifunguliwa tena ni ile ya kitamaduni kwelekea Ukingo wa Magharibi na mashariki mwa Jerusalem.

Hospitali za mashariki mwa Jerusalema na Ukingo wa Magharibi zipo tayari kupokea wagonjwa. Peeperkorn alisema kwamba chini ya makubaliano ya sitisho la mapigano, hadi wagonjwa 50 wa Kipalestina wakiwa wa wenzao wanaweza kuokolewa kutoka Gaza kila siku.

Kufikia sasa hawajaweza kuokoa zaidi ya wagonjwa 39 kwa siku. Amesema kuwa ni lazima hali iimarishwe kwa wagonjwa 12,000 hadi 14,000 wanaohitaji kuokolewa wakiwemo watoto 5,000. Baadhi ya wagonjwa wapo kwenye hali ya mshituko, matatizo ya moyo na wengine saratani.

Forum

XS
SM
MD
LG