Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 14:50

Waziri mkuu wa Mauritius avunja bunge na kuitisha uchaguzi mkuu


Waziri Mkuu wa Mauritius, Pravind Kumar Jugnauth
Waziri Mkuu wa Mauritius, Pravind Kumar Jugnauth

Waziri Mkuu wa Mauritius Pravind Kumar Jugnauth Jumapili alilivunja bunge la nchi hiyo na kusema kwamba kisiwa hicho cha Bahari la Hindi kitafanya uchaguzi mkuu mnamo Novemba 7.

Nchi hiyo, ambayo ni maarufu kwa utalii na moja wapo ya mataifa imara zaidi barani Afrika, hufanya uchaguzi kila baada ya miaka mitano, na wa mwisho ulifanyika mnamo 2014.

Kisheria, Wananchi wa Mauritius wana kati ya siku 30 hadi 150 kushiriki uchaguzi baada ya waziri mkuu kuvunja bunge.

Jugnauth, mwenye umri wa miaka 57, ambaye pia ni waziri wa Fedha atawania muhula mwingine kama kiongozi wa chama kinachotawala cha MSM.

Amehudumu kama Waziri Mkuu tangu mwaka 2017 wakati alipochukua madaraka kutoka kwa baba yake, Anerood Jugnauth.

-Imetayarishwa na Mwandishi wetu Washington DC

XS
SM
MD
LG