Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Februari 11, 2025 Local time: 01:47

Waziri wa fedha wa Marekani anasema kuongeza msaada kwa Ukraine, 'ni njia bora' ya kuimarisha uchumi wa dunia


Waziri wa fedha wa Marekani Janet Yellen akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kabla ya mkutano wa mawaziri wa fedha wa nchi za G20, kwenye ukumbi wa Mahatma Mandir mjini Gandhinagar, India, Julai 16, 2023.
Waziri wa fedha wa Marekani Janet Yellen akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kabla ya mkutano wa mawaziri wa fedha wa nchi za G20, kwenye ukumbi wa Mahatma Mandir mjini Gandhinagar, India, Julai 16, 2023.

Waziri wa fedha wa Marekani Janet Yellen Jumapili amesema kuongeza msaada kwa Ukraine inayokumbwa na vita ndiyo njia “moja bora” ya kusaidia uchumi wa dunia, pamoja na kukuza uchumi wa nchi zinazojiimarisha na kukabiliana na tatizio sugu la madeni.

Yellen pia alisema pembeni ya mkutano wa mawaziri wa fedha wa nchi za G20 nchini India, atakanusha ukosoaji kuwa kuna malumbano kati ya misaada kwa Ukraine na mataifa yanayoendelea.

“Kukomesha vita hivi kwanza kabisa ni jambo la kimaadili,” aliwaambia waandishi wa habari mjini Gandhinagar.

“Lakini ni jambo bora zaidi tunaweza kufanya kwa uchumi wa dunia,” aliongeza.

Yellen pia alisisitiza juhudi za kukabiliana na tatizo sugu la madeni lyanayoyakabili mataifa yenye uchumi mdogo, mageuzi ya benki na makubaliano ya ushuru wa kimataifa, na akaonya kuwa ni “mapema”kuzungumzia juu ya kuondoa ushuru kwa China.

Forum

XS
SM
MD
LG