Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Machi 29, 2024 Local time: 02:05

Waziri wa biashara wa Uingereza azuru Taiwan


Waziri wa Uingereza Greg Hands kwenye picha ya maktaba
Waziri wa Uingereza Greg Hands kwenye picha ya maktaba

Uingereza imetangaza Jumatatu kwamba imemtuma waziri wa biashara nchini Taiwan, ikiwa ziara  ya kwanza ya moja kwa moja tangu kutokea kwa janga la corona, kwa lengo la kuimarisha uhusiano wa kiuchumi kati ya mataifa yote  mawili.

Ziara hiyo hata hivyo imekemewa vikali na China. Waziri huyo wa Uingereza Greg Hands atakuwa mmoja wa viongozi katika mazungumzo hayo ya kila mwaka, huku pia akitarajiwa kukutana na rais wa kisiwa hicho, Tsai Ing-wen wakati wa ziara hiyo ya siku mbili.

Taarifa zimeongeza kusema kwamba, sawa na Taiwan, Uingereza inazingatia sheria za soko huru la kimataifa. Msemaji kutoka kwenye ofisi ya kibalozi za Uingereza nchini Taiwan ameliambia shirika la habari la AFP kwamba shughuli rasmi za Hands zitaanza Jumanne.

Taiwan katika miezi ya karibuni imepokea wageni mashuhuri wa kimataifa, miongoni mwao akiwa spika wa bunge la Marekani Nancy Pelosi, aliyezua malalamiko makali kutoka Beijing. China imekuwa ikidai kukimiliki kisiwa hicho kinachojitawala kidemokrasia, wakati ikitishia kukichukua kwa nguvu ikiwezekana.

XS
SM
MD
LG