Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Aprili 25, 2024 Local time: 11:14

Waziri wa afya wa Senegal afutwa kazi, baada ya watoto wachanga 11 kuuawa na moto katika hospitali


Rais wa Senegal Macky Sall akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa uwanja wa michezo huko Diamniadio, nje ya mji mkuu Dakar, February 22, 2022. Picha ya AFP
Rais wa Senegal Macky Sall akitoa hotuba wakati wa ufunguzi wa uwanja wa michezo huko Diamniadio, nje ya mji mkuu Dakar, February 22, 2022. Picha ya AFP

Rais wa Senegal Macky Sall Alhamisi amemfuta kazi waziri wake wa afya, Abdoulaye Diouf Zarr, amri ya serikali imeonyesha, baada ya watoto wachanga 11 kuuawa na moto katika chumba cha hospitali cha watoto wachanga.

Nafasi ya Sarr itachukuliwa na Marie Khemesse Ngom Ndiaye, mkurugenzi mkuu wa wizara ya afya, kwa mujibu wa amri hiyo ya serikali.

Maafisa wanasema hitilafu ya umeme ndio ilisababisha moto kuzuka Jumatano jioni na kuua watoto hao wachanga katika hospitali ya mji wa magharibi mwa Senegal wa Tivaouane.

Rais Macky Sall ametoa taarifa ya msiba huo kwenye Twitter na kutangaza siku tatu za maambolezo ya kitaifa.

Meya wa mji wa Tivaouane Demba Diop amesema moto huo ulisababishwa na hitilafu ya umeme na ulisambaa kwa haraka sana.

Amekanusha madai ya ndugu wa watoto hao kwenye hospitali na kwenye mitandao ya kijamii kwamba watoto hao wachanga walikuwa wameachwa peke yao, akisema mkunga na muuguzi walikuwepo Jumatano jioni.

XS
SM
MD
LG