Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Julai 26, 2026 Local time: 12:11

61 wauwawa, 150 wajeruhiwa katika shambulizi la kujitoa muhanga Pakistan

Picha ya maktaba
Picha ya maktaba

Bomu lenye nguvu lililipuka katika msikiti uliokuwa na waumini wengi kaskazini magharibi mwa Pakistan, Jumatatu na kuua watu 61, na kujeruhi zaidi ya watu 150 wengine.

Shambulizi la mchana katikati mwa Peshawar, mji mkuu wa jimbo la Pakhtunkhwa, lilifanywa nje na mjitoa muhanga kwa mujibu wa polisi.

Afisa wa juu wa polisi wa Peshawar aliithibitishia kwa VOA idadi ya wote waliofariki dunia, inaweza kuongezeka na bado kuna waumini ambao bado hawaja hesabiwa na miili haijatambuliwa.

Afisa wa juu wa usalama, naibu kamishina Shafiullah Khan, amesema watu wawili walio nusurika walikutwa katika kifusi.

Maafisa wa hospitali wa mji walithibitisha kupokea dazeni ya walio jeruhiwa, na kuelezea hali zao kuwa ni mbaya. Walio athirika wengi wao waliokuwa ni polisi wa jimbo.

This item is part of
XS
SM
MD
LG