Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Machi 28, 2023 Local time: 21:21

61 wauwawa, 150 wajeruhiwa katika shambulizi la kujitoa muhanga Pakistan


Picha ya maktaba

Bomu lenye nguvu lililipuka katika msikiti uliokuwa na waumini wengi kaskazini magharibi mwa Pakistan, Jumatatu na kuua watu 61, na kujeruhi zaidi ya watu 150 wengine.

Shambulizi la mchana katikati mwa Peshawar, mji mkuu wa jimbo la Pakhtunkhwa, lilifanywa nje na mjitoa muhanga kwa mujibu wa polisi.

Afisa wa juu wa polisi wa Peshawar aliithibitishia kwa VOA idadi ya wote waliofariki dunia, inaweza kuongezeka na bado kuna waumini ambao bado hawaja hesabiwa na miili haijatambuliwa.

Afisa wa juu wa usalama, naibu kamishina Shafiullah Khan, amesema watu wawili walio nusurika walikutwa katika kifusi.

Maafisa wa hospitali wa mji walithibitisha kupokea dazeni ya walio jeruhiwa, na kuelezea hali zao kuwa ni mbaya. Walio athirika wengi wao waliokuwa ni polisi wa jimbo.

Facebook Forum

XS
SM
MD
LG