Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Aprili 18, 2026 Local time: 12:18

Watu zaidi waokolewa wakiwa hai Uturuki

Waokoaji nchini  Uturuki waliwatoa watu zaidi wakiwa hai katika vifusi Jumatatu zaidi ya wiki moja baada ya kutokea mfululizo wa matetemeko ya ardhi yaliyolikumba eneo hilo.

Licha ya mafanikio hayo, matumaini yanapotea kwamba kuna waathirika zaidi watapatikana wakiwa hai.

Katika mji wa kusini mwa Islahiye, katika jimbo la Gaziantep, waokoaji waliwamtoa mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 40, wakati katika jimbo la kusini la Hatay, msichana mwenye umri wa miaka 13 aliokolewa baada ya kukaa kwa saa 182 chini ya kifusi ambapo tukio hilo liliwafanya waokoaji kushangilia.

Televisheni ya Uturuki ililionyesha eneo la tukio la watu wengine kadhaa wakiwa wanaokolewa Jumatatu, lakini wataalamu wameonya kwamba muda unazidi kwenda na kuwa vigumu kuwapata watu wakiwa hai katika majengo ambayo yameanguka.

This item is part of
XS
SM
MD
LG