Upatikanaji viungo

Breaking News
Ijumaa, Januari 17, 2025 Local time: 07:47

Watu wawili wauawa nchini Bangladesh katika maandamano ya kuipinga serikali


Polisi wa Bangladesh wafyatua risasi za mpira ili kuwatawanya wafuasi wa chama cha upinzani cha BNP, waliokuwa wanajaribu kufunga barabara kuu ya Araihazar, Oktoba 31, 2023.
Polisi wa Bangladesh wafyatua risasi za mpira ili kuwatawanya wafuasi wa chama cha upinzani cha BNP, waliokuwa wanajaribu kufunga barabara kuu ya Araihazar, Oktoba 31, 2023.

Watu wawili wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa leo Jumanne nchini Bangladesh katika mapambano kati ya polisi na waandamanaji wanaoipinga serikali, siku ya kwanza ya maandamano ya siku tatu ya kumshinikiza waziri mkuu Sheikh Hasina kujiuzulu.

Chama kikuu cha upinzani, Bangladesh National Party (BNP) kimeomba barabara zifungwe kwa siku tatu kufuatia mapambano ya siku ya Jumapili kati ya wafuasi wake na polisi ambapo afisa mmoja wa polisi aliuawa na zaidi ya watu 100 kujeruhiwa.

Chama hicho kimemuomba waziri mkuu Sheikh Hasina ajiuzulu ili kuruhusu uchaguzi uliopangwa mwezi Januari ufanyike chini ya serikali ya mpito isiyoegemea upande wowote. Lakini serikali ya waziri mkuu ilipinga ombi hilo.

Forum

XS
SM
MD
LG