Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumamosi, Februari 08, 2025 Local time: 19:27

Watu 54 wauwawa katika shambulizi Sudan


Mashambulizi ya wanamgambo wa Sudan, yameuwa watu 54 katika soko la mji mkuu pacha wa Omdurman, Jumamosi kwa mujibu wa chanzo cha madakatari kilichozungumza na shirika la habari la AFP.

Mfanyakazi wa hospitali ya karibu ya Al-Nao, akiomba kutotajwa, amesema idadi ya waliofariki ni kubwa katika tukio ambalo inadaiwa limefanywa na wanamgambo wa kikosi cha akiba (RSF).

Toka Aprili 2023, wanamgambo wa RSF wamekuwa kwenye vita na jeshi la Sudan, katika mzozo mbaya ambao umeua maelfu ya watu na kuwafanya watu zaidi ya milioni 12 kukosa makazi.

Mhudumu wa kujitolea katika Hospitali ya Al-Nao, ameiambia AFP kwamba walikuwa wakihitaji sana sanda, wachangiaji damu na machela ili kuwasafirisha waliojeruhiwa.

Hospitali hiyo ni mojawapo ya vituo vya mwisho vya matibabu vinavyofanya kazi katika eneo hilo, na imekuwa ikishambuliwa mara kwa mara.

Forum

XS
SM
MD
LG