Chombo cha habari cha serikali cha ORTM kimesema kwamba gurudumu la lori hilo lilipasuka na kusababisha dereva wake kushindwa kulidhibiti na ndipo liliserereka upande wa basi na kugongana ana kwa ana.
Shirika la habari la Reuters linasema kuwa ajali hiyo ilitokea kiasi cha kilomita 20 kutoka mji wa Segou ambako sehemu ya mbele ya basi hiyo iliharibiwa kabisa kulingana na picha na video zilzowekwa mtandaoni.
Msemaji wa wizara ya uchukuzi Mohamedoune Ould Mamouni ameongeza kusema kuwa watu 33 walijerujiwa wakati wa ajali hiyo. Kulingana na takwimu kutoka shirika la afya duniani WHO, Afrika ndiyo yenye bara bara hatari zaidi ulimwenguni ambapo vifo 26 kutokana na ajali kutokea kwa kila idadi ya watu 100,000.