Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumatatu, Juni 16, 2025 Local time: 07:09

Watu 21 wauawa nchini Niger katika shambulio la kigaidi.


Ramani ya Niger.
Ramani ya Niger.

Watu wanaoshukiwa kuwa wanajihadi walishambulia basi na lori nchini Niger na kuua watu 21 katika eneo la kusini magharibi la Tillaberi, karibu na Burkina Faso, vyanzo vya eneo hilo na vya usalama vimesema.

Chanzo kimesema “ Shambulio la kigaidi la Jumatano alasiri ambalo lilifanywa na watu wenye silaha nzito waliokuwa kwenye pikipiki na ndani ya gari liliua watu 19 waliokuwa wanasafiri kwa basi, mkiwemo afisa wawili wa polisi”.

Chanzo hicho kimeongeza kuwa watu wengine wawili waliuawa katika shambulio dhidi ya lori ambalo lilichomwa moto na washambuliaji.

Watu watano akiwemo afisa moja wa polisi walijeruhiwa katika shambulio dhidi ya basi ambalo nalo lilichomwa moto.

XS
SM
MD
LG