Maafisa wa eneo hilo wameripoti matukio ya mauaji ya kiholela yaliyofanywa na watu wenye silaha huko Diallassagou na miji miwili jirani katika eneo la Bankass, eneo la Sahel ambalo limekuwa lenye machafuko kwa muda mrefu.
"Walichoma pia vibanda, nyumba na kuiba ng'ombe," amesema afisa wa eneo hilo ambaye hakutaka jina lake litajwe kwa sababu za kiusalama.
Yeye na afisa mwingine ambao wote wawili walikimbia kijiji chao, wamesema hesabu ya watu waliouawa ilikuwa ikiendelea Jumatatu.
Nouhoum Togo, afisa wa mji wa Bankass, mji mkubwa katika eneo hilo, amesema idadi ya waliouawa ni kubwa kuliko ile ya watu 132 iliyotangazwa na serikali, ambayo iliwashtumu wanamgambo wa kiislamu washirika wa Al-Qaeda kwa mauaji hayo.