Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumanne, Mei 14, 2024 Local time: 09:38

Watu 1,300 wa Myanmar wamekimbilia Thailand


Takriban watu 1,300 wamekimbia kutoka mashariki mwa Myanmar kuelekea Thailand, maafisa wamesema Jumamosi, wakati mapigano mapya yakizuka katika mji wa mpakani ambao hivi karibuni ulitekwa na wapiganaji wa msituni wa kikabila.

Wapiganaji kutoka kabila la walio wachache la Karen wiki iliyopita waliiteka ngome ya mwisho ya jeshi la Myanmar ndani na kuzunguka Myawaddy, ambayo imeungana na Thailand kwa madaraja mawili katika Mto Moei.

Mapigano ya karibuni kabisa yalizuka asubuhi wakati wapiganaji wa msituni wa Karen walipoanzisha mashambulizi dhidi ya wanajeshi wa Myanmar waliokuwa wamejificha karibu na daraja la pili la urafiki la Thailand na Myanmar, kivuko kikuu cha biashara na Thailand, alisema mkuu wa polisi Pittayakorn Phetcharat katika wilaya ya Mae Sot nchini Thailand.

Alikadiria kuwa akriban watu 1,300 walikimbilia Thailand.

Forum

XS
SM
MD
LG