Mgogoro uliozuka mwezi Aprili kati ya wanajeshi watiifu kwa mkuu wa jeshi la Sudan, Abdel Fattah al-Burhan, na kikosi cha dharura (RSF) vya Jenerali Mohamed Hamdan Daglo, una matokeo makubwa ya kibinadamu, kiusalama, kiuchumi na kisiasa ambayo ni masuala yenye kuzua wasiwasi mkubwa kwa utawala wa kisiasa wa Wasudan Kusini, alisema mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Pembe ya Afrika, Hanna Tetteh.
Pamoja na mashambulizi yake ya kijeshi huko Kordofan Magharibi na kutwaa uwanja wa ndege wa Belila na visima vya mafuta, RSF inakaribia Abyei, ikidhibiti sehemu za mpaka na Sudan Kusini, Tetteh alisema wakati wa mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Forum