Upatikanaji viungo

Breaking News
Jumapili, Machi 16, 2025 Local time: 02:06

Washambuliaji waua watu wawili Israel nao wakauawa baadaye.


Polisi wa Israel wakifanya ulinzi kwenye eneo la tukio la shambulizi la kisu katika mji wa zamani wa Jerusalem, Machi 18, 2018. Picha ya AP.
Polisi wa Israel wakifanya ulinzi kwenye eneo la tukio la shambulizi la kisu katika mji wa zamani wa Jerusalem, Machi 18, 2018. Picha ya AP.

Washukiwa wawili Waarabu wenye silaha wameua watu wawili Jumapili nchini Israel, na baadaye nao wakauawa, huduma ya gari la kubeba wagonjwa imesema.

Mauaji hayo yametokea wakati waziri wa mambo ya nje wa Marekani na mawaziri wengine wa mambo ya nje kutoka nchi za kiarabu wakifanya ziara nchini humo kwa ajili ya mkutano wa kilele.

Hakuna kundi lililodai kuhusika katika ufyatuaji huo wa risasi katika mji wa Hadera, ulioko umbali wa kilomita 50 kaskazini mwa Tel Aviv.

Tukio hilo linajiri siku 5 baada ya raia mmoja muarabu wa Israel kuua watu wanne kwa kuwachoma kisu katika mji wa kusini wa Beersheba, kabla ya kuuawa kwa kupigwa risasi na mpita njia.

Video ya kamera ya ulinzi iliyopeperushwa kwenye vituo vya televisheni vya Israel imeonyesha watu wawili wakifyatua risasi na bunduki za kushambulia kwenye barabara kuu ya Hadera.

XS
SM
MD
LG