Upatikanaji viungo

Breaking News
Alhamisi, Februari 13, 2025 Local time: 09:34

Wapalestina watatu wauawa katika shambulio la jeshi la Israel


Wapalestina watizama nyumba zao zilizoharibiwa katika shambulizi la Israel wakati wa mapigano kati ya Israel na Gaza, Mei 14, 2023.
Wapalestina watizama nyumba zao zilizoharibiwa katika shambulizi la Israel wakati wa mapigano kati ya Israel na Gaza, Mei 14, 2023.

Wapalestina watatu waliuawa mapema Jumatatu katika shambulio la jeshi la Israel kwenye kambi ya wakimbizi huko Ukingo wa Magharibi, maafisa wa afya wa Palestina wamesema, huku utawala wa Biden ukilaani vikali kitendo cha hivi karibuni cha Israel kuendelea kuteka makazi ya Wapalestina.

Wizara ya afya ya Palestina imesema wanaume watatu waliuawa wakati wa shambulio huko Balata, ambako kuna kambi ya wakimbizi karibu na mji wa Nablus. Watu sita walijeruhiwa, akiwemo mtu mmoja ambaye yuko katika hali mahututi, wizara hiyo imesema.

Jeshi la Israel lilithibitisha baadaye kwamba wanajeshi walilishambulia eneo la Balata. Limesema wanajeshi walishambuliwa kwa risasi na waliwaua Wapalestina watatu.

Jeshi limeongeza kuwa watu wengine watatu walikamatwa.

Hata hivyo, utawala wa Biden ulitoa taarifa yenye maneno makali Jumapili, ukiikosoa Israel kwa kuendelea kuweka tena makazi ya walowezi katika kituo cha zamani cha Homesh kaskazini mwa Ukingo wa Magharibi.

XS
SM
MD
LG